8. Taji Mvikeni
1. Ni tabibu wa karibu;
Tabibu wa ajabu;
Na rehema za daima;
Ni dawa yake njema.
Imbeni, malaika,
Sifa za Yesu Bwana;
Pweke limetukuka
Jina lake Yesu.
2. Hatufai kuwa hai,
Wala hatutumai,
Ila kweli yeye ndiye
Atupumzishaye.
3. Dhambi pia na hatia
Ametuchukulia;
Twendeni na amani
Hata kwake Mbinguni.
4. Huliona tamu jina
La Yesu Kristo Bwana,
Yuna sifa mwenye kufa
Asishindwe na kufa.
5. Kila mume asimame,
Sifa zake zivume;
Wanawake na washike
Kusifu jina lake.
6. Na vijana wote tena,
Wapendao sana
Waje kwake wawe wake
Kwa utumishi wake.
Comments
Post a Comment