8. Taji Mvikeni


1. Ni tabibu wa karibu;
Tabibu wa ajabu;
Na rehema za daima;
Ni dawa yake njema.

 Imbeni, malaika,
 Sifa za Yesu Bwana;
 Pweke limetukuka
 Jina lake Yesu.

2. Hatufai kuwa hai,
Wala hatutumai,
Ila kweli yeye ndiye
Atupumzishaye.

3. Dhambi pia na hatia
Ametuchukulia;
Twendeni na amani
Hata kwake Mbinguni.

4. Huliona tamu jina
La Yesu Kristo Bwana,
Yuna sifa mwenye kufa
Asishindwe na kufa.

5. Kila mume asimame,
Sifa zake zivume;
Wanawake na washike
Kusifu jina lake.

6. Na vijana wote tena,
Wapendao sana
Waje kwake wawe wake
Kwa utumishi wake.

Comments

Popular posts from this blog

6. Baba Mwana Roho

2. Twamsifu Mungu

26. Yesu Unipendaye