5. Jina Lake Yesu Tamu


1. Jina lake Yesu tamu;
Tukilisikia
Hutupoza, tena hamu
Hutuondolea.

2. Roho iliyoumia
Kwalo hutibika,
Chakula, njaani pia;
Raha, tukichoka.

3. Jina hili ni msingi,
Ngao, ngome, mwamba,
Kwa hili napata wingi,
Kwangu ni akiba.

4. Yesu, Mchunga, Rafiki
Mwalimu, Kuhani,
Mwanzo, Mwisho, Njia, Haki,
Uzima kifoni.

5. Moyo wangu hauwezi,
Kukusifu kweli,
Ila sifa zangu hizi,
Bwana zikubali.

6. Na utakaponiita,
Kuja kwako Bwana,
Huko kwako sitaacha
Kukusifu sana.

Comments

Popular posts from this blog

6. Baba Mwana Roho

2. Twamsifu Mungu

26. Yesu Unipendaye