3. Hata ndimi elfu


1. Hata ndimi elfu elfu,
Hazitoshi kweli
Bwana Yesu kumsifu,
Kwa zake fadhili.

2. Yesu, jina liwezalo
Kufukuza hofu;
Lanifurahisha hilo,
Lanipa wokovu.

3. Jina hilo ni uzima;
Ni afya amani;
Laleta habari njema;
Twalipiwa deni.

4. Yesu huvunja mapingu
Ya dhambi moyoni;
Msamaha, tena nguvu,
Twapata rohoni.

5. Kwa sauti yake vile
Wafu hufufuka
Wakafurahi milele,
Pasipo mashaka.

6. Ewe Yesu wangu Bwana,
Uwezo nipewe,
Kuhubiri kote sana,
Wote wakujue.

Comments

Popular posts from this blog

6. Baba Mwana Roho

2. Twamsifu Mungu

26. Yesu Unipendaye