3. Hata ndimi elfu
1. Hata ndimi elfu elfu,
Hazitoshi kweli
Bwana Yesu kumsifu,
Kwa zake fadhili.
2. Yesu, jina liwezalo
Kufukuza hofu;
Lanifurahisha hilo,
Lanipa wokovu.
3. Jina hilo ni uzima;
Ni afya amani;
Laleta habari njema;
Twalipiwa deni.
4. Yesu huvunja mapingu
Ya dhambi moyoni;
Msamaha, tena nguvu,
Twapata rohoni.
5. Kwa sauti yake vile
Wafu hufufuka
Wakafurahi milele,
Pasipo mashaka.
6. Ewe Yesu wangu Bwana,
Uwezo nipewe,
Kuhubiri kote sana,
Wote wakujue.
Comments
Post a Comment