22. Kale Nilitembea


1. Kale nilitembea
Nikilemewa dhambi
Nilikosa msaada,
kuniponya mateso.

 Usifiwe Msalaba!
 Lisifiwe kaburi!
 Linalozidi yote,
 Asifiwe Mwokozi!

2. Hata nilipofika,
Mahali pa Msalaba,
Palinifaa sana,
Sitasahau kamwe.

3. Hicho ndicho chanzo,
Cha kufurahi kwangu.
Hapo ndipo mzigo,
Uliponituliwa.

4. Panapo msalaba,
Kinatolewa cheti,
Cha kuingia Mbinguni,
Kisicho cha kanisa.

5. Yule Bwana mjinga,
Likwenda bila cheti,
Kitumai kwingia,
Kama walio nacho.

6. Lipofika langoni,
Akaulizwa cheti,
Cha kumwonyesha Bwana,
Akakutwa hanacho.

7. Lituhuzunishalo,
Ni ninyi msio nacho,
Kuwa kama mjinga,
Kwa siku ya arusi!

8. Ubavuni mwa Yesu,
Mlitokea damu,
Chemchemi ya uzima,
Itakasayo roho.

9. Jitahidi wingie,
Damuni mwa Mwokozi,
Utafutiwa dhambi,
Toka rohoni mwako.

Comments

Popular posts from this blog

6. Baba Mwana Roho

2. Twamsifu Mungu

26. Yesu Unipendaye