20. Ninaye Rafiki Naye


1. Ninaye Rafiki naye
Alinipenda mbele;
Kwa kamba za pendo zake
Nimefungwa milele;
Aukaza moyo wangu,
Uache mageule,
Mimi wake, yeye wangu;
Ndimi naye milele.

2. Ninaye rafiki ndiye
Aliyenifilia;
Alimwaga damu yake
Kwa watu wote pia;
Sina kitu mimi tena,
Nikiwa navyo tele;
Pia vyote ni amana
Ndimi wake milele.

3. Ninaye rafiki naye
Uwezo amepewa;
Atanilinda mwenyewe,
Juu tachukuliwa;
Nikitazama Mbinguni,
Hupata nguvu tele;
Sasa natumika chini,
Kisha juu milele.

4. Ninaye rafiki naye,
Anao moyo mwema;
Ni mwalimu, kiongozi,
Mlinzi wa daima;
Ni nani wa kunitenga
Na mapenzi ya mbele?
Kwake nimetia nanga,
Ndimi wake milele.

Comments

Popular posts from this blog

2. Twamsifu Mungu

6. Baba Mwana Roho

7. Ni Tabibu Wa Karibu