18. Akifa Yesu Nikafa Naye


1. Akifa Yesu nikafa naye
Uzima upya huishi naye;
Humtazama mpaka aje:
Nyakati zote ni wake yeye.

 Nyakati zote nimo pendoni,
 Nyakati zote ni uzimani,
 Humtazama hata atokee,
 Nyakati zote mimi ni wake.

2. Vita sipigi visivyo haki,
Na Bwana wangu hapiganiki;
Beramu yake haitwaliki,
Napo po pote hila sitaki.

3. Sina mashaka, akawa mbali;
Mizigo yote aihimili;
Ananituliza Imanweli,
Nyakati zote mimi husali.

4. Sina huzuni na mimi sidhii;
Simwagi chozi, wala siguni;
Sikuti afa, ila kitini
Daima hunifikiri mimi.

5. Kila unyonge huusikia;
Kila ugonjwa kwake hupoa;
Yesu ni mwenye kuniokoa
Nyakati zote hunijalia.

Comments

Popular posts from this blog

6. Baba Mwana Roho

2. Twamsifu Mungu

26. Yesu Unipendaye