17. Namwandama Daima



1. Namwndama Bwana kwa alilonena
Njia yangu huning’azia;
Nikimridhisha atanidumisha
Taamini nitii pia.

 Amini utii, njia pweke ni hii
 Ya furaha kwa Yesu: amini ukatii.

2. Giza sina kwangu wala hata wingu
Yeye mara huviondoa
Woga, wasiwasi, sononeko, basi;
Huamini nitii pia.

3. Masumbuko yote, sikitiko lote;
Kwa mapenzi hunilipia;
Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki
Taamini nitii pia.

4. Mimi sitajua raha sawasawa
Ila yote Yesu kumpa;
Napata fadhili na radhi kamili,
Taamini nitii pia.

5. Nitamfurahia na kumtumaini,
Majumbani na njia-njia;
Agizo natenda, nikitumwa hwenda,
Huamini nitii pia

Comments

Popular posts from this blog

6. Baba Mwana Roho

2. Twamsifu Mungu

26. Yesu Unipendaye