12. Ewe Roho Wa Mungu


1. Ewe Roho wa Mbinguni
Uje kwetu sasa.
Ufanye makazi yako
Ndani ya Kanisa.

2. Ndiwe mwanga, umulike
Tupate jikana;
Mengi kwetu yapunguka,
Tujalize, Bwana.

3. Ndiwe Moto, teketeza
Taka zetu zote:
Moyo na iwe sadaka
Ya Mwokozi, yote.

4. Ndiwe Umande, na kwako
Tutaburudika,
Nchi kavu itakuwa
Ni yenye Baraka.

5. Roho wa Mbinguni uwe
Nasi hapa chini,
Mwili uufananishe
Na kichwa Mbinguni.

Comments

Popular posts from this blog

6. Baba Mwana Roho

2. Twamsifu Mungu

26. Yesu Unipendaye