11. Nina Haja Nawe



1. Nina haja nawe
Kila saa;
Hawezi mwingine
Kunifaa.

 Yesu, nakuhitaji
 Vivyo kila saa!
 Niwezeshe, Mwokozi,
 Nakujia.

2. Nina haja nawe;
 Kaa nami,
 Na maonjo haya,
 Hayaumi.

3. Nina haja nawe;
 Kila hali,
 Maisha ni bure,
 Uli mbali.

4. Nina haja nawe,
 Nifundishe
 Na ahadi zako
 Zifikishe.

5. Nina haja nawe,
 Mweza yote,
 Ni wako kabisa
 Siku zote.

Comments

Popular posts from this blog

6. Baba Mwana Roho

2. Twamsifu Mungu

26. Yesu Unipendaye